SIMCHIMBA HASHIKIKI LIGI YA CHAMPIONSHIP YA NBC

 

IKIWA imesalia mechi moja pekee kwa kila timu ya Ligi ya Championship ya NBC ufungaji wa mabao umeendelea kushika kasi huku mchezaji wa Geita Gold ya mkoani Geita Andrew Simchimba akiendelea kuongoza akiwa na mabao 18 katika mechi 22 alizocheza.

Nafasi ya pili inashikiliwa na mchezaji Abdulaziz Shahame wa TMA ya mkoani Arusha akiwa na mabao 17 huku timu yake ikishika nafasi ya sita baada ya kukusanya alama 50.

Mchezaji Raizin Hafidh wa Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro anashika nafasi ya tatu akiwa amefunga mabao 16 huku timu yake ikiwa imekata tiketi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26.

Nafasi ya nne ipo kwa mchezaji Ambokile Eliud wa Mbeya City ya mkoani Mbeya akiwa na mabao 11 huku akiisaidia timu yake kurejea tena kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu ujao.

Yusuph Mhilu wa timu ya Geita Gold anafunga ‘Mkeka’ akishika nafasi ya tano na mabao 10 huku Geita ikishika nafasi ya nne na ikitarajiwa kucheza michezo ya mtoano kuwania kucheza Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *