KIVUMBI CHA LIGI KUU YA NBC KUENDELEA LEO.

IKIELEKEA siku za mwisho za msimu wa 2024/25 Ligi Kuu ya NBC inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo mmoja utakaokutanisha timu ya Simba itakayokuwa uwanja wa nyumbani wa KMC Complex dhidi ya Pamba Jiji kutoka Mwanza.

Simba iliyoshinda mchezo wake uliopita kwa bao moja ugenini dhidi ya JKT Tanzania inarudi uwanjani leo kucheza na Pamba Jiji iliyolazimishwa sare ya 1-1 nyumbani dhidi ya Fountain Gate.

Pamba inaingia kwenye mchezo wa leo ikiwa timu namba tatu kwa kushinda michezo michache ikishinda sita, nyuma ya Kagera iliyoshinda mitano na KenGold iliyoshinda mitatu.

Simba inaingia kwenye mchezo wa leo akiwa imepoteza mchezo mmoja pekee huku ikiwa timu iliyoruhusu mabao machache hadi sasa kwenye Ligi Kuu ya NBC ikifungwa tisa.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *