MICHEZO mitatu ya Ligi ya Championship ya NBC inapigwa leo Machi 17 ambapo mikoa ya Geita, Mbeya na Shinyanga itakuwa wenyeji wa michezo hiyo.
Michezo ya Leo inazikutanisha baadhi ya timu zinazopambana kujiweka vizuri kwenye nafasi nne za juu za msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC.
Stand United iliyo nafasi ya tatu na alama 46 itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar iliyo nafasi ya kwanza na alama 54 kwenye uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga.
Mkoani Geita, Geita Gold inayoshika nafasi ya nne ikiwa na alama 45 itakuwa mwenyeji wa Mbeya Kwanza iliyo nafasi ya sita na alama 39 kwenye uwanja wa Nyankumbu.
Mchezo wa Mwisho leo utazikutanisha Mbeya City inayoshika nafasi ya pili dhidi ya Kiluvya iliyo nafasi ya 12 kwenye uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya huku michezo yote ya Leo itaanza kuanzia majira ya saa 10:00 za alasiri.