NYASI ‘KUWAKA’ MOTO LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC leo inatimua vumbi kwa michezo miwili itakayopigwa kwenye viwanja vya Sokoine, Mbeya na Kaitaba, Kagera.

Mchezo wa saa 10:00 alasiri utakuwa kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Coastal Union ambapo Prisons inahitaji kushinda mchezo wa leo ili kujiondoa kwenye nafasi ya kucheza michezo ya mtoano.

Endapo Prisons inayoshika nafasi ya 14 itashinda itafikisha alama 30 na itakuwa nyuma ya Coastal Union inayoshika nafasi ya nane kwa tofauti ya alama moja pekee.

Mchezo wa mwisho utapigwa mkoani Kagera kwenye uwanja wa Kaitaba saa 12:30 jioni kati ya Kagera Sugar dhidi ya Mashujaa.

Kagera inayoshika nafasi ya 14 inahitaji kushinda mchezo wa leo ili kufufua matumaini ya kusalia Ligi Kuu ya NBC msimu 2025/26 huku Mashujaa ikihitaji alama tatu muhimu kujihakikishia nafasi ya kusalia kwenye ligi hiyo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *