SIMBA YAJIPATA LIGI KUU YA NBC.

Timu ya Simba imerudi kwenye njia ya ushindi kwa kuifunga Prisons bao moja baada ya kudondosha pointi 5 katika michezo miwili ya Ligi Kuu ya NBC kwa kutoa sare na timu ya Coastal Union na kufungwa na Yanga katika mchezo wa Derby ya Kariakoo .

Simba jana ikiwa jijini Mbeya ilifanikiwa kuifunga timu ya Prisons dakika ya tano ya mchezo huo lililofungwa na mlinzi wa kati wa Simba Che Malone baada ya kipa wa Prisons Musa Mbisa kushindwa kuudaka mpira wa faulo.

Baada ya mchezo huo simba ilifikisha alama 16 sawa na timu ya Fountain Gate huku Simba ikiwa nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu tofauti ya mabao ya kufungwa Simba ikiruhusu mabao 3 na Fountain Gate wakiruhusu mabao 13.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *