RUVU KUJIULIZA KWA STAND , MBUNI, POLISI VITA NBC CHAMPIONSHIP LEO

Ligi ya NBC Championship inaendelea leo Novemba 17 kwa michezo miwili kwenye mikoa miwili tofauti.

Mchezo wa saa 8:00 Mchana Stand United watawaalika Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga.

Stand ipo nafasi ya 10 kwenye msimamo ikicheza jumla ya michezo 10 na kupata ushindi kwenye michezo mitatu, sare tatu na kufungwa minne huku ikikusanya alama 12.

Ruvu Shooting ipo nafasi ya mwisho kwenye msimamo baada ya kucheza jumla ya michezo 10 ikifungwa michezo 9 na kupata sare mchezo mmoja ikiwa haijashinda mchezo wowote na kuwa na alama moja.

Mchezo wa pili utazikutanisha Mbuni dhidi ya Polisi Tanzania saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Black Rhino, Karatu.

Mbuni ipo nafasi ya nne ya Msimamo baada ya kucheza michezo 10 na kushinda mitano wakitoa sare mitatu na kufungwa miwili huku wakikusanya Alama 18 na Polisi wakishika nafasi ya sita kwenye msimamo ikicheza jumla ya michezo 10 ikitoa sare michezo miwili na kufungwa michezo mitatu na kuwa na jumla ya alama 17.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *