YANGA YAMALIZA HATUA YA MAKUNDI KOMBE LA MAPINDUZI NA SULUHU.

 

Mwakilishi wa Ligi Kuu ya NBC Yanga amemaliza michezo yake ya hatua ya makundi ya Kombe la Mapinduzi kwa suluhu dhidi ya KVZ.

Yanga amemaliza kinara wa kundi C baada ya kushinda michezo miwili na kupata sare mchezo mmoja hivyo kufikisha jumla ya alama saba ambazo hakuna timu katika kundi hilo ambayo inaweza kufikia alama hizo.

Baada ya matokeo hayo Yanga anafuzu moja kwa moja katika hatua ya Robo fainali ya Kombe hilo linaloendelea kwenye uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *