KOMBE la Mapinduzi linaendelea leo visiwani Zanzibar kwa mchezo wa ‘miamba’ ya Ligi Kuu ya NBC kati ya Simba na Singida Fountain Gate saa 2:15 katika uwanja wa New Amaan Complex.
Simba na Singida FG wapo Kundi B katika michuano hiyo ya Mapinduzi ambapo Simba ana alama 3 baada ya kucheza mchezo mmoja huku Singida FG akiwa na alama 6 baada ya kucheza michezo miwili na kushinda yote.
Mchezo huo unawakutanisha wawakilishi wawili kati ya wanne wa Ligi Kuu ya NBC katika Kombe hilo la Mapinduzi