YANGA KUIPEPERUSHA BENDERA YA LIGI KUU YA NBC KOMBE LA MAPINDUZI LEO.

 

KOMBE la Mapinduzi linaendelea leo huko Visiwani Zanzibar, saa 2:15 usiku wawakilishi wengine wa Ligi Kuu ya NBC Yanga watakukatana KVZ katika mchezo wa mwisho wa kundi C.

Yanga wanaongoza kundi hilo wakiwa na alama sita baada ya michezo miwili huku KVZ wakiwa na alama nne baada ya michezo miwili.

Jana mchezo wa wawakilishi wawili wa Ligi kuu ya NBC Simba dhidi ya Singida FG ulimalizika kwa simba kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa sifuri, mabao ya Simba yalifungwa na Willy Onana na Luis Miquissone.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *