SIMBA YAENDELEA ILIPOISHIA, MTIBWA, COASTAL HAKUNA MBABE.

TIMU ya Simba imepata ushindi wa pili mfululizo katika Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Dodoma Jiji kwa mabao 2-0 na Kukwea kileleni mwa msimamo kwa mara ya kwanza msimu huu.

Dodoma iliyoanza Ligi vema msimu huu kwa kuifunga Coastal Union mabao 2-1 imeshindwa kutamba mbele ya ‘Mnyama’ kwa mabao yaliyofungwa na Jean Baleke kipindi cha kwanza na Moses Phiri kipindi cha pili.

Mabao hayo yanaifanya Simba iliyofunga mabao sita kuwa kinara kwa kufunga mabao msimu huu mpaka sasa.

Mkoani Morogoro timu ya Mtibwa imeshindwa kutamba kwa mara nyingine ikiwa nyumbani baada ya kutoka sare ya 1-1 na Coastal Union ya Tanga.

Bao la mpira wa adhabu lililofungwa na Ibrahim Ajibu kwa Coastal na bao la Kassim Haruna yamefanya timu hizo kutoshana nguvu na kuendelea kusubiri kwa michezo inayofuata kupata ushindi wa kwanza msimu huu.

Ligi Kuu ya NBC itaendelea tena Agosti 21, kwa mchezo mmoja kati ya Mashujaa itakayokuwa mwenyeji wa Geita Gold saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *