TIMU ya Geita Gold imeendelea kung’ara ikicheza ugenini baada ya kupata suluhu dhidi ya Mashujaa kwenye uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.
Geita imeanza vema Ligi Kuu ya NBC kwa kukusanya alama nne katika michezo miwili bila kuruhusu bao lolote tofauti na msimu uliopita waliporuhusu mabao manne katika michezo miwili ya mwanzo.
Mashujaa iliyopanda daraja msimu huu imeshinda mchezo mmoja dhidi ya Kagera Sugar na suluhu ya leo inaifanya timu hiyo kufikisha alama nne na kukaa nafasi ya pili ya msimamo wa ligi nyuma ya Simba.
Ligi Kuu ya NBC itaendelea tena Agosti 22 kwa mchezo mmoja kati ya Singida Big Stars na Tanzania Prisons utakaochezwa uwanja wa Liti, Singida saa 10:00 alasiri.