TIMU ya Tabora United imeendelea na wimbi la matokeo mazuri ikicheza uwanja wa nyumbani baada ya Leo kuifunga Dodoma Jiji mabao 2-1 katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora.
Tabora imekusanya jumla ya alama nane na kushika nafasi ya tano huku ikiwa timu ya tatu kwa kufunga mabao mengi kwenye uwanja wa nyumbani (matano) sawa na timu ya Azam.
Timu ya Azam imepanda kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kuifunga Coastal Union bao 1-0 kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.
Bao pekee na la ushindi la Azam limefungwa na Feisal Salum dakika 44 ya mchezo.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa michezo miwili Kati ya KMC na Ihefu saa 10 alasiri katika uwanja wa Uhuru, Dar huku mchezo wa pili utazikutanisha Geita Gold dhidi ya Yanga saa 10:00 alasiri katika uwanja wa CCM Kirumba mkoani Mwanza.