SIMBA YANGURUMA DAR,GEITA YATAKATA MBEYA

TIMU ya Simba imefanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Namungo FC likifungwa na Moses Phiri dakika ya 32 kipindi cha kwanza baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Mohammed Hussein ‘Zimbwe Junior’.

Matokeo hayo yanaifanya Simba kufikisha pointi 24 na kukalia nafasi ya pili nyuma ya vinara Azam FC wenye alama 26 huku Namungo ikisalia nafasi ya saba na pointi 15.

Bao lililofungwa na Moses Phiri Linamfanya afikishe Mabao sita akizidiwa bao moja na kinara Sixtus Sabilo anaekipiga timu ya Mbeya City mwenye mabao saba.

Mkoani Morogoro majira ya saa nane mchana timu ya Mtibwa Sugar imefanikiwa kubaki na alama zote tatu nyumbani baada ya kuifunga Coastal Union ya Tanga mabao 2-1 mchezo uliopigwa uwanja wa Manungu.

Mabao ya Mtibwa yamefungwa na Adam Adam dakika ya pili na Juma Nyangi dakika ya 32 huku bao la Coastal likifungwa na Mubarack Amza dakika ya 13.

Matokeo hayo yanaifanya timu ya Mtibwa kufikisha pointi 18 na kupanda nafasi ya tano huku Coastal wakisalia na pointi 12 na kukamata nafasi ya 11 katika msimamo wa Ligi Kuu NBC.

Nayo timu ya Geita Gold imefanikiwa kupata karamu ya mabao mkoani Mbeya baada ya kuwafunga maafande wa Prisons mabao 4-2 mchezo uliopigwa uwanja wa kumbukumbu Sokoine.

Mabao ya Geita yamefungwa na Yusuph Kagoma, Danny Lyanga, Shown Oduro na Edmund John huku mabao ya Prisons yakifungwa na Oscar Paul pamoja na bao la kujifunga kwa Shawn Oduro.

Matokeo hayo yanaifanya Geita kukusanya pointi 17 na kukamata nafasi ya sita katika msimamo wa Ligi huku Prisons ikisalia na pointi 14 na kukamata nafasi ya 10 katika msimamo wa Ligi Kuu NBC.

Ligi hiyo itaendelea Leo kwa michezo mitatu katika mikoa miwili tofauti,Mkoani Mbeya Ihefu SC itaikaribisha Polisi Tanzania uwanja wa Highland Estate majira ya saa nane mchana huku majira ya saa 10 alasiri Mbeya City itaikaribisha Kagera Sugar uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine na mchezo wa saa moja usiku utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa timu ya Yanga itaikaribisha Singida Big Stars mchezo wa mwisho kukamilisha mzunguko wa 12 .

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *