SIMBA YATAKATA ZANZIBAR.

 

MCHEZO wa Ligi Kuu ya NBC Mzizima ‘DERBY’ umemalizika hapa Visiwani Zanzibar Simba ikiibuka na ushindi wa mabao 0-2 dhidi ya Azam FC.

Mabao Leonel Ateba na Fabrice Ngoma yalitosha kuipa alama tatu Simba SC mbele ya Azam FC huku Mlinda Mlambo wa Simba SC Mousa Camara akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa Mchezo.

Kwa matokeo hayo Simba inapanda mpaka nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu ya NBC ikifikisha alama tisa huku Azam FC ikishuka mpaka nafasi ya nne.

Historia mpya imeandikwa kwenye Ligi Kuu kwenye mchezo wa Mzizima ‘Derby’ kuwa ndiyo mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu kuchezwa visiwani Zanzibar.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *