SINGIDA YABANWA NYUMBANI LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Singida Black Stars imepata sare ya kwanza kwenye Ligi Kuu ya NBC baada ya kutoka 1-1 dhidi ya JKT Tanzania.

Singida iliyoshinda michezo minne mfululizo ilikuwa ya kwanza kuandika bao kupitia kwa Elvis Rupia mapema kipindi cha kwanza kabla ya Wilson Nangu kusawazisha kwenye kipindi cha pili.

Hii ni sare ya nne kwa timu ya JKT Tanzania ikiungana na timu za Tanzania Prisons na Pamba kuwa timu zenye sare nyingi kwenye Ligi Kuu ya NBC mpaka sasa.

Sare hiyo inaifanya Singida kufikisha alama 13 sawa na Fountain Gate huku Singida ikiongoza Ligi Kuu ya NBC kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *