MWAKILISHI pekee wa Ligi Kuu ya NBC kimataifa timu ya Simba imefanikiwa kutinga fainali baada ya kuiondoa timu ya Stellenbosch kutoka Afrika Kusini kwa matokeo ya jumla kwa bao 1-0.
Simba imelazimisha suluhu ugenini kwenye uwanja wa Moses Mabhida na kufanikiwa kufuzu baada ya faida ya ushindi wa 1-0 iliyopata kwenye mchezo wa nyumbani uliopigwa uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Simba imefanikiwa kutinga fainali hiyo ya kombe la Shirikisho kwa mara ya kwanza kwenye historia huku ikiwa timu ya pili kutoka kwenye Ligi Kuu ya NBC kufuzu fainali hiyo ndani ya miaka mitatu ikiungana na Young Africans iliyofanya hivyo mwaka 2023.
Simba itakutana na RS Berkane ya Morocco kwenye fainali hiyo iliyofuzu baada ya kuifunga CS Constantine ya Algeria kwa ushindi wa jumla kwa mabao 4-1.
Simba itaanzia ugenini Morocco Mei 17 huku mchezo wa pili na wa mwisho katika shindano hilo ukitarajiwa kupigwa Mei 25 kwenye uwanja wa Mkapa, Dar.
Nawatakia ushindi mnono tim ya simba