HAYA HAPA MABORESHO RATIBA YA LIGI KUU YA NBC

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imefanya maboresho ya ratiba ya Ligi Kuu ya NBC kuanzia mzunguko wa 28 hadi 30 ikiwa ni ratiba ya kukamilisha msimu wa 2024/2025.

Michezo nane ya mzunguko wa 28 inataarajiwa kuchezwa kuanzia mei 12 hadi mei 14 huu timu ya Simba ikicheza dhidi ya Singida Black Stars mei 28 ikiwa ni baada ya mchezo wao wa Fainali ya Kombe la Shirikisho.

Michezo yote nane ya mzunguko wa 29 wa Ligi Kuu ya NBC itachezwa June 18 saa 10:00 alasiri na michezo ya mzunguko wa 30 itapigwa June 22 ambayo itakuwa siku ya kuhitimisha msimu wa 2024/2025.

2 comments

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *