LIGIKUU ya NBC inarejea leo Februari 2 baada ya kusimama kwa takribani siku 40 kupisha fainali za mataifa ya Afrika.
Mchezo mmoja utapigwa leo Kagera Sugar ikiikaribisha Yanga kwenye uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera saa 10:00 alasiri.
Kagera Sugar inaingia kwenye huu mchezo ikiwa nafasi ya 14 kwenye msimamo baada ya kukusanya alama 13 kwenye michezo 13 huku Yanga ikiwa nafasi ya pili baada ya kujikusanyia alama 30 kwenye michezo 11.
Kagera inashuka uwanjani ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo wake uliopita wa Ligi Kuu ya NBC kwa mabao 4-0 dhidi ya Azam nyumbani huku Yanga ikishinda mchezo wake uliopita kwa bao 1 lililofungwa na Stephane Aziz Ki dhidi ya Tabora United ugenini.