Ratiba ya Ligi Kuu ya NBC 2025/2026

TAARIFA YA KAMATI YA UENDESHAJI NA USIMAMIZI WA LIGI YA BODI YA LIGI KUU TANZANIA (TPLB).

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Aprili 26, 2025 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;

Timu ya Tanzania Prisons ya mkoani Mbeya imepewa adhabu ya Onyo Kali kwa kosa la wawakilishi wa timu kuchelewa kwa dakika 12 kuwasili kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo (MCM) kinyume na matakwa ya kanuni ya 17:2 (2.1).Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 194: Tanzania Prisons 1-0 Kagera Sugar

Klabu ya Tanzania Prisons ya mkoani Mbeya imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la watoto waokota mipira (Ball Kids) kuficha na kuchelewesha kwa makusudi kurejesha mipira kiwanjani.

Kuanzia dakika ya 63 ya mchezo, watoto hao walikuwa wakificha mipira inayotoka hali iliyosababisha hadi kufika dakika ya 80 ya mchezo uwe umesalia mpira mmoja pekee kiwanjani.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 195: Pamba Jiji 1-0 Tabora United

Klabu ya Tabora United ya mkoani Tabora imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kukataa kutumia chumba maalum cha kuvalia kwa kile walichoeleza kuwa kulikuwa na harufu isiyo ya kawaida.

Kamishna pamoja na Mratibu wa mchezo huo waliwasiliana na Daktari wa mchezo ili kuthibitisha hali hiyo lakini aliwaeleza kuwa harufu hiyo ilikuwa ya Sabuni zilizotumika kufanyia usafi katika vyumba vyote (kikiwemo chumba cha timu mwenyeji).Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 200: Singida BS 1-0 Azam FC

Kocha Mkuu wa Klabu ya Azam FC Rachid Taoussi ameadhibiwa kwa kutozwa faini yaSh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuwafanyia vurugu na kuwarushia chupa ya maji waamuzi wa mchezo tajwa hapo juu mara baada ya mchezo huo kutamatika.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 45:2(2.1) ya ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Makocha.

Mechi Namba 202: Pamba Jiji 1-1 Fountain Gate

Klabu ya Fountain Gate imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kukataa kutumia chumba maalum cha kuvalia kwa kile walichoeleza kuwa chumba hicho kilikuwa na joto, uamuzi ambao waliufanya bila kumshirikisha Afisa yeyote wa mchezo.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Ligi ya Championship ya NBC

Mechi Namba 195: Green Warriors 2-3 Polisi Tanzania

Klabu ya Polisi Tanzania ya mkoani Kilimanjaro imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la kuchelewa kufika kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo. Meneja wa timu ya Polisi Tanzania Maliki Warioba alifika kwenye kikao saa 4:25 huku viongozi wengine wakifika saa 4:35 badala ya saa 4:00 ambapo walikuta kikao kimefungwa.

Kuchelewa kwenye Kikao cha Maandalizi ya mchezo ni kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo.

Mechi Namba 201: Kiluvya FC 0-1 Mbeya Kwanza

Klabu ya Mbeya Kwanza ya mkoani Mtwara imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la kuwakilishwa na maofisa wanne (4) badala ya watano (5) kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo

Mechi Namba 203: Mtibwa Sugar 2-1 Mbuni FC

Klabu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la maofisa wake wawili kutokuvaa sare za timu kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2(2.10) ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo

Mechi Namba 207: Songea United 1-2 Stand United

Klabu ya Songea United ya mkoani Ruvuma imeadhibiwa kwa kupewa Onyo kali kwa kosa la kuchelewa kuwasili uwanjani. Songea United waliwasili uwanjani saa 8:45 mchana badala ya saa 8:30 mchana kinyume na kanuni ya 17:15 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo

Mechi Namba 214: Geita Gold 2-1 Songea United

Klabu ya Songea United ya mkoani Ruvuma imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la kuchelewa kufika kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo. Wawakilishi timu ya Songea United walifika kwenye kikao saa 4:07 badala ya saa 4:00.Kuchelewa kwenye Kikao cha Maandalizi ya mchezo ni kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo.

First League

Mechi Namba 54A: Pan African 1-1 Nyumbu FC

Daktari wa klabu ya Nyumbu, Alex Theodory amefungiwa kwa kipindi cha mwezi moja (1) na kutozwa faini ya Sh. 300,000 (laki tatu) kwa kosa la kumtolea lugha ya matusi mwamuzi wa kati wa mchezo tajwa hapo juu.

Daktari huyo alifanya kitendo hicho kisicho cha kiuanamichezo wakati wa mchezo huo na aliadhibiwa pia kwa kadi nyekundu na mwamuzi wa mchezo.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 47:3 ya First League kuhusu Udhibiti kwa Viongozi.

Mechi Namba 56A: Dar City 3-0 Tunduru Korosho

Klabu ya Tunduru Korosho ya mkoani Ruvuma imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la wawakilishi wake kushindwa kuhudhuria kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo. Kutokufika kwenye Kikao cha Maandalizi ya mchezo ni kwenda kinyume na Kanuni ya 18:2 (2.2) ya First League kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 18:60 ya First League kuhusu Taratibu za mchezo.

Mechi Namba PO1: Tunduru Korosho 2-2 Mapinduzi FC

Meneja wa klabu ya Mapinduzi, David Kinasa amefungiwa kwa kipindi cha mwezi moja (1) na kutozwa faini ya Sh. 300,000 (laki tatu) kwa kosa la kumtolea lugha ya matusi mwamuzi wa mchezo.

Kinasa alifanya kitendo hicho kisicho cha kiuanamichezo wakati wa mchezo huo na aliadhibiwa pia kwa kadi nyekundu.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 47:3 ya First League kuhusu Udhibiti kwa Viongozi.

 

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *