MKOANI Tabora leo Juni 16 unapigwa mchezo wa marudiano kutafuta ushiriki wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025 unaozikutanisha timu za Tabora United na Biashara United.
Mchezo huu utapigwa kuanzia saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Ali Hassani Mwinyi, Tabora na kurushwa Mbashara na Azam Tv kupitia chaneli ya Azam Sports 1 HD.
Mchezo wa Kwanza uliopigwa katika uwanja wa Karume mkoani Mara ulimalizika kwa Biashara kuibuka na Ushindi wa Bao moja lililofungwa na Herbert Lukindo dakika ya 90+9 kupitia mkwaju wa penati.
Mshindi wa Jumla kwenye michezo hii miwili atashiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025.