JUMLA ya mabao 517 yamefungwa kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/2024 huku rekodi ya bao la mapema zaidi ikishikiliwa na Mudathir Yahya.
Mudathir Yahya alifunga bao hilo sekunde ya 44 dhidi ya KMC mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro ukitumika Kama uwanja wa nyumbani wa KMC.
Mabao mengine ya mapema yalifungwa na Sospeter Bajana wa Azam FC sekunde ya 54 kwenye mchezo dhidi ya JKT Tanzania.
Yassin Mgaza wa Dodoma jiji, Awesu Awesu wa KMC na Ibrahim Ajibu wa Coastal Union wote wamefunga bao kwenye dakika ya kwanza.
Yassin mgaza akifunga dhidi ya Tabora UTD, Awesu Awesu akifunga dhidi Mashujaa na Ibrahim Ajibu akifunga dhidi Dodoma Jiji.