TABORA, COASTAL KUKIWASHA LEO, AZAM KUJIULIZA NYUMBANI.

TIMU ya Tabora United iliyopo kwenye muendelezo mzuri wa matokeo leo inashuka dimbani kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora dhidi ya Coastal union ya Tanga saa 10:00 alasiri.

Tabora inaingia uwanjani leo ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kupata matokeo ya ushindi wa mabao 2-1 kwenye mchezo wake uliopita nyumbani dhidi ya Azam ya Dar es Salaam.

Coastal inakutana na Tabora ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo uliopita ugenini dhidi ya Fountain kwa mabao 3-2 kwenye uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara.

Mchezo wa mwisho leo utakuwa kati ya Azam FC dhidi ya Fountain Gate FC kwenye uwanja wa Azam Complex, Dar saa 1:00 usiku.

Azam itajaribu kupata ushindi leo ikiwa ni baada ya kupoteza mchezo uliopita ugenini dhidi ya Tabora United huku Fountain ikijaribu kuendeleza matokeo mazuri ya ushindi baada ya kushinda mchezo uliopita dhidi ya Coastal nyumbani.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *