Tag: #COSMOPOLIAN

MZUNGUKO WA 17 NBC CHAMPIONSHIP KUKAMILIKA LEO.

MZUNGUKO wa 17 wa Ligi ya Championship ya NBC unatamatika leo kwa mchezo kati ya Transit Camp ya Dar es salaam na Stand United ya Shinyanga saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Mabatini Mkoani Pwani.

Transit Camp ipo nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 10 sawa na Kiluvya iliyo nafasi ya 14 zikitofautiana kwenye mabao ya kufunga na kufungwa huku Stand United ikiwa nafasi ya nne (4) na alama 32.

Mpaka sasa Mtibwa Sugar inaongoza kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 44 kwenye michezo 17 wakati Biashara United ikishika nafasi ya mwisho ikiwa na alama nne (4) pekee kwenye michezo 17

STAND YAILIZA KILUVYA,MBUNI YAJIPATA KWA POLISI NBC CHAMPIONSHIP

LIGI ya NBC Championship Mzunguko wa 16 leo imeendelea kwa michezo minne ya mwisho ya mzunguko huo iliyochezwa viwanja mbalimbali nchini  kuanzia majira ya saa nne  asubuhi  na saa kumi jioni.

Bigman waliwakaribisha Mbeya City katika uwanja wa Ilulu mkoani Lindi saa nne asubuhi baada ya mchezo huo kuahirishwa kuchezwa jana kutokana na mvua iliyonyesha mkoani Lindi  na kusababisha uwanja kujaa maji.

Katika mchezo huo Bigman walifanikiwa kuchukua alama 3 kutoka kwa Mbeya City na kufikisha alama 25 katika msimamo wa Ligi hiyo wakiwa nafasi ya saba  baada ya mchezaji wao Francis Kapeta kufunga bao pekee kwa mkwaju wa penati hivyo mchezo kumalizika 1-0.

Mchezo mwingine ulichezwa majira ya saa kumi jioni ambapo timu ya Stand United waliwakaribisha timu ya Kiluvya katika uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

Dakika ya saba ya mchezo huo Stand United walifungua akaunti ya mabao kupitia mchezaji wao Lukas Sendama na dakika kumi baadae Adam Uledi aliongeza bao la pili hivyo kuwafanya Stand United kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao mawili.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo Kiluvya walifanikiwa kupata bao dakika ya 66 ya mchezo huo kupitia mchezaji wao Hassan Bundala na dakika ya 82 Sendama alirudi tena nyavuni hivyo kuwafanya Stand United kuchukua alama zote tatu na mchezo kumalizika kwa 3-1, Stand United wamepanda hadi nafasi ya nne wakiwa na alama 32.

Kwa upande wa mechi ya Mbuni dhidi ya  timu ya Polisi Tanzania iliyochezwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha mechi ilianza saa kumi alasiri.

Katika mchezo huo Mbuni walifanikiwa kupata bao dakika ya 33 ya mchezo huo kupitia mchezaji Malulu Thomas kabla ya Hassan Rishedy kuongeza bao la pili dakika ya 44 hivyo Mbuni  hivyo matokeo kubaki hivyo hadi mwisho wa mchezo huo  2-0 hivyo kufikisha alama 23 huku wakiwa nafasi ya tisa kakika msimamo.

Timu ya Transit Camp waliwakaribisha  timu ya Biashara United kutoka mkoani Mara kwenye uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi Mkoani Pwani

Katika mchezo huo Biashara United walifanikiwa kubeba alama tatu baada ya mchezaji wao Timotheo Abubakar kufunga bao dakika ya 28 ya mchezo huo ambao ulitamatika  kwa matokeo ya 0-1 hivyo Biashara kufanikiwa kupata alama tatu mhimu wakifikisha alama 4 huku wakiwa wa mwisho katika msimamo wa Ligi hiyo.

TMA YAJIPATA KWA GEITA GOLD NBC CHAMPIONSHIP

LIGI ya NBC Championship Mzunguko wa 16 ulianza jana januari 24 kwa michezo ilicho  na leo imeendelea kwa mchezo mmoja uliochezwa mkoani Arusha Katika Uwanja wa Sheikh Amri  Abeid majira ya  saa kumi jioni.

Katika mchezo huo timu ya TMA waliwakaribisha Geita Gold ambapo mchezo ulianza kwa timu zote kushambuliana kwa kasi  kubwa ambapo mpaka mapumziko hakuna aliyeweza kutikisa nyavu za mwenzake.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kubwa ambapo TMA walifanikiwa kupata bao la kwanza ikiwa ni dakika ya 50 ya mchezo huo  kupitia mchezaji wao Abdul Shahame kabla ya Kasimu Shaibu kuongeza bao  la pili dakika ya 61 ya mchezo huo .

Dakika ya 72 ya mchezo huo Geita Gold walifanikiwa kupata goli lao la kwanza kupitia mchezaji wao Masanja Jesto  hivyo matokeo kuwa 2-1 ambayo yalisalia mpaka mwisho wa mchezo huo.

Baada ya mchezo huo kutamatika TMA alifanikiwa kufikisha pointi 30 hivyo kupanda hadi nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi hiyo kutoka nafasi ya sita alipokuwa awali.

Ligi ya NBC Championship itaendelea kesho kwa michezo minne Bigman dhidi ya Mbeya City ulioahirishwa kuchezwa leo kutokana na mvua kubwa kunyesha katika uwanja wa Ilulu Lindi,Stand United dhidi ya Kiluvya,Transit Camp dhidi ya Biashara United na Mbuni dhidi ya Polisi Tanzania.