MZUNGUKO wa 17 wa Ligi ya Championship ya NBC unatamatika leo kwa mchezo kati ya Transit Camp ya Dar es salaam na Stand United ya Shinyanga saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Mabatini Mkoani Pwani.
Transit Camp ipo nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 10 sawa na Kiluvya iliyo nafasi ya 14 zikitofautiana kwenye mabao ya kufunga na kufungwa huku Stand United ikiwa nafasi ya nne (4) na alama 32.
Mpaka sasa Mtibwa Sugar inaongoza kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 44 kwenye michezo 17 wakati Biashara United ikishika nafasi ya mwisho ikiwa na alama nne (4) pekee kwenye michezo 17
 
					 
		 
		