LIGI KUU ya NBC inaendelea leo Novemba 6 kwa michezo miwili kwenye Mikoa miwili tofauti kati ya Mashujaa wakiwaalika Singida BS kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mkoani kigoma na Geita Gold dhidi ya Tabora United kwenye uwanja wa Nyankumbu, Geita huku michezo yote ikianza saa 10:00 alasiri.
Mashujaa wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza michezo mitatu mfululizo ya Ligi Kuu ya NBC.
Geita Gold inashika nafasi ya 15 kwenye msimamo baada ya kucheza michezo minane ikishinda mmoja, ikisuluhu michezo mitatu na kufungwa mitano hivyo kukusanya alama sita.
Tabora United ipo nafasi ya nane ikishinda michezo miwili,
sare michezo minne na kufungwa mitano hivyo kuwa na alama 10 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.