UCHAGUZI MDOGO BODI YA LIGI KUU TANZANIA RASMI DISEMBA 9.

Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Imetangaza uchaguzi mdogo wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania utakaofanyika Disemba 9, 2023 Jijini Dar es Salaam.

Nafasi zinazogombewa ni Mjumbe mwakilishi wa Klabu za Ligi Kuu ya NBC na Mjumbe mwakilishi wa Klabu za NBC Championship huku Mgombea lazima awe Rais au Mwenyekiti wa Klabu.

Fomu za uchaguzi zitatolewa kuanzia Oktoba 13 hadi 17 katika Ofisi za TFF na tovuti ya TFF na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania, Gharama za fomu ni Sh.100,000 (Laki moja) za kitanzania.

@election press TPLB

election calendar TPLB 2023

Fomu No. 1 ya uchaguzi TPLB

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *