Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo Machi 9 kwa michezo mitatu kuchezwa kwenye mikoa mitatu tofauti.
Mkoani Morogoro Mtibwa Sugar itaialika Tanzania Prisons saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Manungu huku timu zote mbili zikipata ushindi kwenye michezo yao iliyopita Mtibwa ikiifunga Singida Fountain Gate huku Tanzania Prisons ikiifunga Simba.
Saa 12:00 jioni Coastal Union itaialika Simba katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.
Mchezo wa kwanza timu hizo zilipokutana kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es salaam Coastal Union ilipoteza mabao 3-0.
Mchezo wa Mwisho kwa leo utazikutanisha Dodoma Jiji dhidi ya Geita Gold saa 2:15 usiku kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma huku Geita Gold ikiwa nafasi ya 15 moja kutoka mwisho na alama 18 huku Dodoma Jiji ikiwa nafasi ya 9 na alama 23 na kuufanya mchezo kuwa wa ushindani.