Ratiba ya Ligi Kuu ya NBC 2025/2026

VIWANJA NANE KAZINI LEO LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC inatimua ‘vumbi’ leo kwenye viwanja nane tofauti ikiwa ni michezo ya kukamilisha mzunguko wa 30 wa ligi hiyo msimu wa 2024/25.

Macho na masikio yatakuwa zaidi kwa ‘Vigogo’ wa ligi hiyo timu za Yanga na Simba zilizopishana alama moja pekee huku timu hizo zikiwa nyumbani kwenye michezo yao ya leo.

Young Africans inayoongoza ligi hiyo itakuwa nyumbani kwenye uwanja wa New Amaan, Zanzibar kuwaalika Dodoma Jiji ya Dodoma huku ‘watani’ zao Simba wakiwa uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam kuwaalika Kagera Sugar iliyoshuka daraja hadi sasa.

‘Maafande’ wa timu ya Mashujaa watakuwa nyumbani kwenye uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma kuwaalika wenzao wa JKT Tanzania huku timu ya Pamba Jiji ya halmashauri ya Jiji la Mwanza ikiwa mwenyeji wa KMC inayomilikiwa na manispaa ya Kinondoni kwenye uwanja wa Nyamagana, Mwanza.

Singida Black Stars itakuwa kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Liti, Singida kuwakaribisha Tanzania Prisons ya Mbeya inayopambana kujitoa kwenye nafasi ya kucheza hatua ya mtoano huku Ken Gold ikiwa ugenini kwenye uwanja wa Majaliwa, Lindi kurusha ‘karata’ yake ya mwisho ya Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Namungo baada ya kushuka daraja msimu huu ikiwa timu ya mwisho kwenye msimamo wa ligi hiyo.

‘Matajiri wa Chamazi’ timu ya Azam FC baada ya kuichapa Tabora United mabao 5-0 nyumbani, itakuwa ugenini leo kwenye uwanja wa Tanzanite Kwaraa dhidi ya Fountain Gate na mchezo wa mwisho utakuwa kati ya Coastal Union ambayo haijapoteza mchezo tangu kurejea kwenye uwanja wake wa Mkwakwani ikiikaribisha Tabora United.

Michezo yote itapigwa kuanzia saa 10:00 alasiri na kurushwa mbashara kwenye stesheni za Azam.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *