NBC CHAMPIONSHIP KUANZA RASMI LEO

PAZIA la Ligi ya NBC Championship msimu wa 2023/2024 linafunguliwa rasmi leo Septemba 9 kwa michezo mitatu kuchezwa katika viwanja mbalimbali.

Mchezo wa kwanza wa ufunguzi utazikutanisha Mbeya City dhidi ya Green Warriors saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Sokoine, Mbeya mchezo wa pili utazikutanisha Mbeya Kwanza dhidi Polisi Tanzania saa 10:00 alasiri katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mkoani Mtwara na mchezo wa mwisho ni kati ya Copco na Pan Africans saa 10:00 alasiri uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Hii ni kwa mara ya kwanza Ligi ya Championship kupata udhamini ambapo Benki ya Taifa ya Biashara, NBC imeandika historia ya kuwa mdhamini wa kwanza na kuifanya Ligi hiyo sasa kutambulika kama Ligi ya NBC Championship.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *