TIMU ya Yanga imeanza Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/24 kwenye uwanja wa Azam Complex, Dar kwa kishindo baada ya kuifunga KMC mabao 5-0.
Dickson Job, Ki Aziz, Hafiz Konkoni, Midathir Yahya, na Pacome Zouzoua ndio walioifanya timu ya Yanga kuwa timu iliyofunga mabao mengi katika mchezo mmoja mpaka sasa katika Ligi Kuu ya NBC msimu huu.
Yanga ilimaliza msimu uliopita kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons na kutwaa ubingwa ikiwa imepoteza michezo miwili pekee dhidi ya Ihefu na Simba.
Ligi hiyo itaendelea tena Agosti 28 kwa mchezo utakaochezwa uwanja wa Azam Complex, Dar kati ya Azam na Tanzania Prisons saa 3:00 usiku.