MABAO 5-1 walioshinda Yanga dhidi ya Simba yametosha kuwabakiza kileleni mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya NBC kwa alama 21 baada ya kucheza mechi tisa.
Mabao yaliyofungwa na Kennedy Musonda, Maxi Nzengeli aliyefunga mawili, Ki Aziz na Pacome Zouzoua yameifanya Simba kuruhusu mabao 10 huku wakifunga 17.
Ushindi huo umeifanya Yanga kufikisha jumla ya mabao 25 kwenye michezo 9 waliyocheza mpaka sasa.
Yanga wamesalia kileleni mwa msimamo wakiwaacha wapinzani wao Simba na pointi zao 18 huku Simba wakiwa wamecheza mechi saba .