KMC NDANI YA TATU BORA LIGI KUU YA NBC.

 

LIGI KUU ya NBC imeendelea Leo kwa Mchezo mmoja katika uwanja wa Uhuru, Dar na kushuhudia KMC akiibuka na Ushindi wa Bao moja dhidi ya Mtibwa Sugar, lililowapeleka mpaka nafasi ya tatu ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Bao pekee na la ushindi kwa KMC limefungwa na Ibrahim Elias Dakika ya 15 ya mchezo na kuifanya KMC kufikisha alama 15 na michezo saba mfululizo bila kupoteza.

Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo mitatu, mapema saa 8:00 Mchana Singida BS watawaalika Ihefu katika uwanja wa Liti mkoani Singida, Mashujaa watawaalika Azam FC saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma na Mchezo wa mwisho saa 1:00 usiku Coastal Union watakuwa wenyeji wa Namungo katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *