TIMU ya Young Africans imefanikiwa kuifunga timu ya Namungo bao moja kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa kwenye uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi.
Mchezo ulianza kwa timu zote kushambuliana kwa kasi kubwa kuhakikisha wanachukua alama tatu za Ligi Kuu ya NBC ili kujiweka katika nafasi nzuri kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu.

Dakika 26 zilimtosha mshambuliaji wa Young Africans Laurindo Dilson kufungua ukurasa wa mabao kupitia mkwaju wa penati baada ya mchezaji wao Max Nzengeli kufanyiwa madhambi na mchezaji wa Namungo bao lililodumu hadi mwisho wa kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili timu zote zilirejea kwa kasi kubwa Namungo ikijaribu kufanya mashambulizi ya mbali ambayo hata hivyo hayakuweza kuzaa matunda hadi dakika 90 za mchezo huo zinatamatika wageni Young Africans walifanikiwa kubeba alama zote tatu kutoka kwa Namungo. Mchezaji Max Nzengeli wa Young Africans alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.
