AZAM YATAKATA KMC COMPLEX.

TIMU ya Azam imeendeleza ubabe wake dhidi ya timu ya KMC baada ya kuifunga 0-2 katika mchezo uliopigwa leo kwenye uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo timu zote zilikuwa zikiutaka mchezo na zilishambuliana kwa kasi licha ya Azam kuutawala mchezo huo lakini hadi dakika 45 zinatamatika hakuna aliyefanikiwa kuguza nyavu za mwenzake kwa bao.

Akaminko (kushoto) akipambana namchezaji wa KMC

Kipindi cha pili dakika ya 55 ya mchezo mchezaji wa Azam Iddy Seleiman alifungua ukurasa wa mabao wa timu hiyo na kurejea tena kambani dakika ya 64 ya mchezo huo na kufanya Azam kuongoza kwa mabao mawili.

Hadi mwamuzi wa mchezo huo Ramadhani Kayoko anapuliza kipenga cha mwisho matokeo yalisalia 0-2 na kuifanya KMC kuendelea kuburuza ‘mkia’ wa Ligi Kuu ya NBC huku Iddy Selemani akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *