VITA ya ufungaji bora inazidi kushika kasi baada ya Kiungo wa Simba, Jean Ahoua, kufikisha mabao 10 sawa na mchambuliaji wa Young Africans, Clement Mzize, ambae ndio kinara wa mabao baada ya kutamatika mzunguko wa 20 wa Ligi Kuu ya NBC.
Ahoua ambae awali alikuwa na mabao nane alifanikiwa kufunga mabao mawili ya penati wakati wa mchezo wa Namungo dhidi ya Simba uliochezwa katika uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi licha ya Simba kuwa na mchezo mmoja wa kiporo dhidi ya Dodoma Jiji ambao uliahirishwa kutokana na timu hiyo kupata ajali.
Nafasi ya tatu ni mshambuliaji wa Young Africans,Prince Dube akiwa na mabao tisa mpaka sasa huku Elvis Rupia wa Singida Black Stars na Leonel Ateba wa Simba wakiwa nafasi ya nne na tano wakiwa na mabao manane kila mmoja.
Kwa upande wa kiungo wa Young Africans Pacome Zouzua na Peter Lwasa wa Kagera Sugar wanashikiria nafasi ya sita na saba huku wakiwa na mabao saba kila mmoja.
Ligi Kuu ya NBC itaendelea kesho ambapo mzunguko wa 21 utaanza kwa michezo miwili ambapo JKT Tanzania watawakaribisha Kagera Sugar uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo Mbeni mkoani Dar es Salaam na Tanzania Prisons wakiwakaribisha Tabora United katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
duh!