DUBE,AHOUA HAPATOSHI UFUNGAJI BORA LIGI KUU NBC.

VITA ufungaji bora imeanza upya ndivyo unavyoweza kusema baada ya mshambuliaji wa Young Africans Prince Dube kumfikia  idadi ya mabao kiungo wa Simba,Jean Ahoua huku Ligi Kuu ya NBC ambayo ni Ligi namba nne kwa ubora barani Africa ikielekea ukingoni.

Dube ambaye amefunga mabao 12 na kutoa pasi za mwisho nane katika michezo 25 ambayo timu yake imeshacheza mpaka sasa katika Ligi Kuu ya NBC sawa na Ahoua wa timu ya Simba ambaye amefanikiwa kufunga mabao 12  na kutoa pasi za mwisho saba katika michezo 22 ambayo timu yake imeshacheza.

Young Africans imebakisha michezo mitano ikiwa imeshacheza michezo 25 huku Simba ikiwa imebakisha michezo minane baada ya kucheza mechi 22 hivyo njia inaweza kuwa nyepesi kwa wachezaji hao na wengine wanaowakaribia kuibuka na ufungaji bora wa Ligi Kuu mara baada ya kufikia ukingoni.

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *