COASTAL UNION WAIZINDUA MKWAKWANI KIBABE LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC inaendelea kushika kasi ambapo jana Coastal Union iliwakaribisha timu ya Singida Black Stars katika uwanja wa Mkwakwani Tanga ikiwa ni mechi ya kwanza tangu kuboreshwa kwa uwanja huo.

Mchezo huo ulianza majira ya saa 10:00 alasiri ambapo timu zote zilikuwa na shauku ya kuchukua alama ili kujiweka katika mazingira mazuri Coastal Union wakiendelea kujinasua kutoka nafasi za chini kwenye msimamo na Singida wakipambania nafasi nne za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Dakika 47 ziliwatosha Coastal Union kuongoza mchezo baada ya kupata bao la kwanza baada ya mchezaji wa Singida Josephat Bada kujifunga hivyo kuwafanya wana mangushi kwenda mapumziko na uongozi wa 1-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na dakika ya 76 mshambuliaji wa Singida, Jonathan Sowah aliipatia timu yake bao kupitia mkwaju wa penati na dakika ya 82 mchezaji wa Coastal union, Bakari Msimu aliongeza bao hivyo mchezo kutamatika kwa 2-1.

Matokeo hayo yanaipeleka Coastal hadi nafasi ya 10 na alama 28 huku Singida ikisalia nafasi ya nne ikiwa na alama 50.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *