Author: Yahaya Abushehe

TANZANIA YAANZA NA USHINDI CHAN 2024.

TANZANIA YAANZA NA USHINDI CHAN 2024.

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imeanza vyema michuano ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza Ligi za ndani CHAN 2024 kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Timu ya Taifa ya Burkina Faso.

Mabao ya Stars yalifungwa na Abdul Suleimani anaekipiga kwenye timu ya Azam ya Dar es Salaam kwa mkwaju wa penati huku la pili likifungwa na Mohammed Hussein aliyemaliza mkataba wake na timu ya Simba akimaliza kazi safi iliyofanywa na Iddy Selemani (Nado) wa Azam.

Mchezo huo ulitanguliwa na Shamra shamra za ufunguzi wa michuano hiyo ambao kwa upande wa burudani ziliongozwa na msanii wa Bongo Fleva Raymond Mwakyusa maarufu Kama ‘Rayvanny’.

Timu ya Tanzania inaundwa na ‘mastaa’ mbalimbali wanaocheza Ligi za ndani ikiwemo Ligi Kuu ya NBC na Ligi ya Championship ya NBC.

Tanzania itarejea tena uwanjani Jumatano ya Agosti 6, saa 2:00 usiku ikiivaa timu ya Taifa ya Mauritania.

NI VITA YA UBINGWA ‘DERBY’ YA KARIAKOO LEO.

 

‘DERBY YA MAAMUZI’ ndivyo unavyoweza kuuita mchezo wa watani wa Jadi ‘Kariakoo Derby’ ndani ya Ligi Kuu ya NBC unachezwa leo saa 11:00 jioni kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam.

Huu ni mchezo wa kufunga Pazia la Ligi Kuu ya NBC kwa msimu wa 2024/2025 lakini pia ndio mchezo utakaotoa Bingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu huu wa 2024/2025.

Young Africans inahitaji alama moja pekee ili kuwa mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu huu kwa kuwa itafikisha alama 80 ambazo haziwezi fikiwa na timu nyengine yoyote.

Matokeo ya Ushindi ndio silaha pekee kwa Simba ili kuweza kuwa mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu huu wa 2024/2025, hii ni kutokana na utofauti wa alama Kati yake na timu inayoongoza Ligi Young Africans.

Yanga inaingia kwenye mchezo huu ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 kwenye mchezo uliopita huku ikiongoza msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 79.

Mwamuzi wa kati kwenye mchezo huu ni Amin Mohammed Amin, mwamuzi msaidizi namba moja ni Mahmoud Ahmed Abo, mwamuzi msaidizi namba mbili Samil Gamal Saad na mwamuzi wa akiba ni Ahmed Mahrous Elghandour wote kutoka Misri.

KARIAKOO DERBY

KARIAKOO ‘DERBY’ KUPIGWA JUNI 25.

BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeusogeza mbele mchezo namba 184 wa Ligi Kuu ya NBC kati ya klabu ya Yanga na klabu ya Simba ambao ulipangwa kufanyika kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Juni 15, 2025 kuanzia saa 11:00 jioni.

Mchezo huo sasa utafanyika Juni 25, 2025 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia saa 11:00 jioni.

Bodi inazitakia maandalizi mema klabu za Yanga na Simba kuelekea mchezo huo.

HATMA YA GEITA, STAND KUJULIKANA LEO .

HATMA ya kucheza mchezo wa mtoano kushiriki Ligi Kuu ya NBC kujulikana leo ambapo timu ya Stand United itakuwa mwenyeji wa Geita Gold kwenye uwanja wa CCM kambarage, Shinyanga saa 10:00 alasiri.

Mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye uwanja wa Nyankumbu ulimalizika kwa Sare ya mabao 2-2 hivyo kuufanya mchezo wa leo kuwa mgumu zaidi timu zote zikitafuta nafasi ya kucheza Ligi Kuu ya NBC.

Ushindi, suluhu au sare ya bao 1-1 unaipa nafasi Stand United kusonga mbele kwenye mchezo wa mtoano unaofuata kwa Faida ya mabao ya ugenini.

Ushindi au sare ya mabao 3-3 na kuendelea unaipa Geita Gold nafasi ya kuendelea kwenye mchezo wa mtoano unaofuata kwa faida ya mabao mengi ya ugenini.

Mshindi wa jumla wa michezo hii ya mtoano wa kupanda (Promotions Playoffs) atacheza na timu iliyofungwa kwenye mchezo wa mtoano utakaozikutaisha timu iliyoshika nafasi ya 13 na 14 kwenye Ligi Kuu ya NBC.

SIMBA, SINGIDA BS KINAPIGWA LIGI KUU NBC LEO.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Mei 28 kwa mchezo mmoja wa kukamilisha mzunguko wa 28 Kati ya Simba na Singida Black Stars katika uwanja wa KMC, Dar es Salaam.

Katika mchezo wa mwisho timu hizo kukutana mkoani Singida timu ya Singida ilikubali kichapo cha bao 0-1 mbele ya Simba kwenye uwanja wake wa Nyumbani CCM Liti bao likifungwa na Fabrice Ngoma.

Simba inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 69 ikishinda michezo 22 ikitoka sare michezo mitatu na kupoteza mchezo mmoja pekee.

Singida Black Stars ipo nafasi ya 4 kwenye msimamo ikiwa na alama 53 baada ya kushinda michezo 16 ikitoka sare mitano na kupoteza michezo sita.