NI VITA YA UBINGWA ‘DERBY’ YA KARIAKOO LEO.

 

‘DERBY YA MAAMUZI’ ndivyo unavyoweza kuuita mchezo wa watani wa Jadi ‘Kariakoo Derby’ ndani ya Ligi Kuu ya NBC unachezwa leo saa 11:00 jioni kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam.

Huu ni mchezo wa kufunga Pazia la Ligi Kuu ya NBC kwa msimu wa 2024/2025 lakini pia ndio mchezo utakaotoa Bingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu huu wa 2024/2025.

Young Africans inahitaji alama moja pekee ili kuwa mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu huu kwa kuwa itafikisha alama 80 ambazo haziwezi fikiwa na timu nyengine yoyote.

Matokeo ya Ushindi ndio silaha pekee kwa Simba ili kuweza kuwa mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu huu wa 2024/2025, hii ni kutokana na utofauti wa alama Kati yake na timu inayoongoza Ligi Young Africans.

Yanga inaingia kwenye mchezo huu ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 kwenye mchezo uliopita huku ikiongoza msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 79.

Mwamuzi wa kati kwenye mchezo huu ni Amin Mohammed Amin, mwamuzi msaidizi namba moja ni Mahmoud Ahmed Abo, mwamuzi msaidizi namba mbili Samil Gamal Saad na mwamuzi wa akiba ni Ahmed Mahrous Elghandour wote kutoka Misri.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *