Author: Yahaya Abushehe

MBEYA STAND NBC CHAMPIONSHIP

MBEYA, STAND VITA YA NAFASI NBC CHAMPIONSHIP LEO.

‘VITA YA NAFASI’ ndivyo unavyoweza kuuita mchezo huu ambapo MBEYA City itaikaribisha Stand United kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya kuanzia saa 10:00 alasiri, kwenye muendelezo wa michezo ya  Ligi ya Championship ya NBC.

Mbeya City ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 52 sawa na Stand United iliyo nafasi ya tatu zikitofautiana kwenye mabao ya kufunga na kufungwa, timu yeyote itakayoshinda mchezo huu itajichukulia kijiti cha nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi hiyo.

MChezo wa mwisho kwa leo utachezwa mkoani Mtwara ambapo Mbeya kwanza ya mkoani hapo itaialika Transit Camp ya Dar es Salaam kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona saa 10:00 alasiri.

GUNNERS HAUSUNG NBC CHAMPIONSHIP.

GUNNERS YAUNGANA NA HAUSUNG NBC CHAMPIONSHIP.

HATIMAYE timu ya Gunners ya mkoani Dodoma imeungana na Hausung ya mkoani Njombe kupanda moja kwa moja Ligi ya Championship ya NBC kwa msimu unaofuata wa 2025/2026 baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mapinduzi na kufikisha alama 35 hivyo kuongoza msimamo wa First League kundi B.

Baada ya kutamatika kwa Ligi hiyo kinachofuata sasa ni mchezo wa kutafuta Bingwa wa First League kwa msimu wa 2024/2025 ambapo kinara kundi A Hausung atakutana na kinara wa kundi B Gunners sambamba na  michezo ya mtoano (PlayOff).

Wakati huo huo timu za African Lyon kutoka kundi A na Ruvu Shooting kutoka Kundi B zimeshuka daraja baada ya kumaliza nafasi za mwisho kwenye makundi yao.

Katika hatua nyengine Ruvu Shooting imekumbana na adhabu ya kushushwa daraja na kufungiwa kushiriki Ligi kwa misimu miwili baada ya ombi lao la kujitoa katika Ligi ya First League kwa kile walichoeleza kuwa ni kushindwa kumudu gharama za uendeshaji kulikosababisha kuondokewa na wachezaji wao kadhaa kukubaliwa na Bodi ya Ligi.

FIRST LEAGUE KUHITIMISHWA LEO.

FIRST LEAGUE KUHITIMISHWA LEO.

LIGI ya First League inahitimishwa leo kwa michezo ya Kundi A na B kwa timu zote kundi A na timu sita kundi B kutupa karata zake kuanzia saa 10:00 jioni,

Tayari timu ya Hausung ya mkoani Njombe imeshakata tiketi ya moja kwa moja  kushiriki Ligi ya championship ya NBC msimu wa 2024/2025 kutoka kundi A huku ikisubiriwa timu ya kupanda moja kwa moja kutoka kundi B ambapo timu za Rhino Rangers, Gunners, na Tanesco zina nafasi kubwa ya kufanya hivyo.

Ikumbukwe kuwa timu inayoshika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa First League Kundi A na B Inafuzu moja kwa moja kushiriki Ligi ya Championship ya NBC.

Wakati timu zinazoshika nafasi ya pili na ya tatu kwenye kila kundi zikicheza michezo ya mtoano (PlayOff) kupata washindi wawili wa kucheza mtoano wa kupanda (Promotion PlayOff) na timu mbili za ligi ya Championship ya NBC.

 

NANI KUMFUATA HAUSUNG NBC CHAMPIONSHIP

NANI KUMFUATA HAUSUNG NBC CHAMPIONSHIP ?

NANI kuungana na Hausung kwenye Ligi ya Championship ya NBC ndiyo swali linalosubiri majibu yake kutoka kundi B la First League ambapo Rhino Rangers, Gunners na Tanesco wanayo nafasi ya kufanya hivyo.

Rhino Rangers ya Tabora ina Jumla ya alama 31 kwenye michezo 13 huku Gunners ya Dodoma ikiwa na alama 29 kwenye michezo 12 wakati Tanesco ya Morogoro ikiwa na alama 26 kwenye michezo 26.

Ikumbukwe kuwa timu inayoshika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa First League Kundi A na B Inafuzu moja kwa moja kushiriki Ligi ya Championship ya NBC.

Wakati timu zinazoshika nafasi ya pili na ya tatu kwenye kila kundi zikicheza michezo ya mtoano (PlayOff) kupata washindi wawili wa kucheza mtoano wa kupanda (Promotion PlayOff) na timu mbili za ligi ya Championship ya NBC.

Wachezaji wa Biashara United wakishangilia bao pekee walilofunga dhidi ya African Sports kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Karume, Mara.

BIASHARA YAFUFUA MATUMAINI MZUNGUKO UKIKAMILIKA NBC CHAMPIONSHIP.

MZUNGUKO wa 23 wa Ligi ya Championship ya NBC umehitimishwa jana kwa mchezo mmoja kuchezwa katika uwanja wa Karume Mkoani Mara na kushuhudia Biashara United ikiibuka na Ushindi wa Bao 1-0 dhidi ya African Sports.

Licha ya Ushindi huo Biashara United inaendelea kusalia nafasi ya mwisho kwenye msimamo ikifikisha alama saba baada ya michezo 23.

Ikumbukwe Biashara United ilipokwa alama 15 baada ya kushindwa kutokea kwenye mchezo dhidi ya Mbeya City.

Mtibwa Sugar inaendelea kusalia kileleni licha ya kupoteza kwenye mchezo wake dhidi ya Stand United ikiwa na alama 54 baada ya michezo 23 ikifuatiwa na Mbeya City na Stand United kwa pamoja zikiwa na alama 49 zikipishana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.