SINGIDA YAONGEZA MAUMIVU KWA MTIBWA.

SINGIDA Black Stars imejipata baada ya kuifunga timu ya Mtibwa Sugar mabao 3-1 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa leo katika uwanja wa Jamhuri Dodoma majira ya saa nane mchana.

Iliwachukua dakika tano pekee Singida kufungua ukurasa wa mabao kupitia mchezaji wao Nduhumwe Mosi na dakika ya 16 Horso Muaku aliiongezea timu hiyo bao la pili hivyo kwenda mapumziko wakiongoza kwa mabao mawili.

Wachezaji wa Singida wakishangilia bao.

Kipindi ca pili timu zote zilikuwa na ari ya kutaka ushindi hasa Mtibwa iliyokuwa nyuma kwa mabao mawili hata hivyo ndoto zao zilizidi kudidimia baada ya Kennedy Juma kuongeza bao la tatu kwa timu ya Singida ikiwa ni dakika ya 58 ya mchezo huo.

Dakika ya 88 Mtibwa ilipata bao la kufutia machozi kupitia mchezaji wao Raizin Haji hivyo kufanya mchezo kumalizika wa 1-3 na Singida kufanikiwa kubeba alama zote tatu ugenini huku mchezaji wa Singida Horso Muaku alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *