LIGI Kuu ya NBC jana iliendelea mkoani Dar es salaam kwa mchezo mmoja uliochezwa Uwanja wa Azam Complex na kushuhudia Azam ikishinda 2-1 dhidi yaSingida Black Stars.
Kiungo wa Azam Feisal Salum alifungua ukurasa wa mabao kwa kufunga bao dakika ya 38 akipokea pasi kutoka kwa Idd Selemani Nado hivyo Azam kwenda mapumziko wakiwa wanaongoza kwa 1-0.
Kipindi cha pili mshambuliaji wa Azam Jhonie Blanco aliiongeza bao la pili timu yake dakika ya 57 ya mchezo huo akipokea pasi kutoka kwa Iddi Seleman .
Dakika ya 62 ya mshambuliaji wa Singida Black Stars Elvis Rupia alifunga bao hivyo kufanya ubao wa matokeo kusomeka 2-1 mpaka mwisho wa mchezo huo .
Mchezaji wa Azam Idd Seleman Nado alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.
Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa michezo miwili kati ya KMC na Tabora United kwenye uwanja wa KMC Complex, Dar na Fountain Gate dhidi ya JKT Tanzania kwenye uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara.