MOTO ULIWAKA LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC ilirejea kwa kasi mwishoni mwa wiki iliyopita kwa michezo iliyochezwa katika viwanja mbalimbali nchini.

Pamba Jiji ya Mwanza ilikuwa mwenyeji wa Simba katika Uwanja wa CCM Kirumba Novemba 22, na Simba kuondoka na alama zote tatu huku mshambuliaji wao Lionel Ateba akitajwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kufunga bao pekee la mchezo huo kwa mkwaju wa penati.

KenGold waliwakaribisha Coastal Union jumamosi ya Novemba 23 katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na kutoka sare ya 1-1 huku bao la Coastal lilifungwa na Abdallah Hassan ambaye pia alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo na Emmanuel Mpuka wa KenGold akisawazisha dakika ya 87 ya mchezo huo.

Mashujaa waliwakaribisha Namungo kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma ambapo Mashujaa waliibuka na ushindi wa bao moja lilifungwa na Abdurahman Mussa huku mchezaji wa Mashujaa Ibrahim Ame alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Azam waliwakaribisha Kagera Sugar jumamosi ya Novemba 23 katika Uwanja wa Azam Complex Dar es Salaam na Azam kuibuka na ushindi wa bao moja lililofungwa na Feisal Salum aliyeibuka mchezaji bora wa mchezo huo .

JKT Tanzania walicheza na Tanzania Prisons katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo Mbweni Dar es Salaam na kuibuka na ushindi wa bao moja lililofungwa na Hassan Kaparata ambaye pia aliyeibuka mchezaji bora wa mchezo huo .

Dodoma Jiji ilikuwa nyumbani kwenye uwanja wa Jamhuri kuwakaribisha KMC na Dodoma kushinda 2-1 huku mabao ya Dodoma yakifungwa na Iddy Kipagwile na Paul Peter ambaye pia alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo na bao la KMC likifungwa na Ali Shaban.

Ligi Kuu itaendelea leo kwa mchezo mmoja uliopaswa kuchezwa jana kati ya Tabora United na Singida Black Stars ambao ulioahirishwa kutokana na uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora kujaa maji baada ya mvua kubwa kunyesha mkoani Tabora.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *