AZIZ KI KINARA WA MABAO LIGI KUU YA NBC.

MCHEZAJI Stephane Aziz Ki wa Yanga amemshusha Jean Baleke wa Simba kwenye msimamo wa vinara wa mabao baada ya kufunga mabao matatu (Hat-trick) dhidi ya timu ya Azam.

Mabao matatu aliyofunga Ki yote kwa mguu wa kushoto yamemfanya kufikisha mabao sita na kumzidi Baleke mwenye matano na Feisal Salum wa Azam mwenye mabao manne.

Matokeo hayo yanaifanya Yanga kufikisha alama 15 sawa na timu ya Simba na kupanda nafasi ya kwanza kwa tofauti ya mabao manne.

Ligi Kuu ya NBC itaendelea tena Oktoba 25 kwa michezo mitatu, JKT Tanzania dhidi ya Tabora United kwenye uwanja wa Azam Complex saa 16:00, Coastal Union na Mashujaa saa 12:30 kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga na mchezo wa mwisho utachezwa uwanja wa Jamhuri saa 21:00 kati ya Dodoma Jiji na Kagera Sugar.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *