LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo ikikutanisha ‘miamba’ wawili wa soka kutoka mkoa wa Dar timu ya Yanga dhidi ya Azam kwenye uwanja wa Mkapa, Dar utakaochezwa saa 12:30 jioni.
Yanga ndiye kinara wa kufunga mabao mpaka sasa (15) huku akiruhusu mabao mawili sawa na Azam.
Azam imeshinda michezo minne mpaka sasa na kutoa sare mmoja ikiwa haijapoteza mchezo wowote huku Yanga ikishinda minne na kupoteza mmoja.
Yanga imeshinda michezo mitano huku Azam ikishinda mitatu na sare tatu zimepatikana miamba hiyo ilipokutana kwenye michezo 10 iliyopita.