MBIO za kuwania kiatu cha ufungaji bora wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/24 zimeendelea kupamba moto huku michezo mitano ikiwa imekamilika kwa kila timu.
Jean Baleke wa Simba ndiye kinara wa ufungaji akiwa na mabao matano huku akifanikiwa kufunga mabao matatu kwenye mchezo mmoja (Hat-Trick) dhidi ya Coastal Union.
Feisal Salum wa Azam anashika nafasi ya pili akiwa na mabao manne huku akiwa amefunga mabao matatu katika mchezo mmoja dhidi ya Tabora United kwenye mchezo wa ufunguzi.
Pacome Zouzoua, Ki Aziz, Maxi Nzengeli wa Yanga na Matheo Anthony wa Mtibwa Sugar wanafuatia nafasi ya tatu wakiwa na mabao matatu kila mmoja.