BIASHARA UNITED YASHUKA FIRST LEAGUE.

TIMU ya Biashara United ya mkoani Mara rasmi imeshuka daraja kutoka Ligi ya Championship ya NBC na msimu ujao 2025/2026 itashiriki ligi ya First League.

Biashara imefikia hatua hiyo baada ya jana Mei 1, kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Geita Gold hivyo kufikisha alama 15 ambazo hata akishinda mchezo wake wa mwisho hazimuondoi katika nafasi ya mwisho ya Ligi ya Championship ya NBC.

Moja ya timu kati ya Transit Camp, Cosmopolitan au African Sports inaweza kuungana na Biashara United kwenye kushuka daraja endapo matokeo yao ya michezo ya mwisho ya Ligi ya Championship ya NBC hayatakuwa mazuri siku ya michezo ya mwisho ya ligi hiyo

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *