SIMBA ‘YATAKATA’ DHIDI YA MASHUJAA LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea leo kwa mchezo mmoja uliochezwa majira ya saa kumi jioni katika uwanja wa KMC mkoani Dar es Salaam ambapo Simba waliwakaribisha timu ya Mashujaa kutoka mkoani Kigoma.

Mchezo ulianza kwa kasi ambapo kila timu ilionyesha ikitaka kupata alama tatu  ambapo iliwachukua dakika tano timu ya Mashujaa kufungua ukurasa wa mabao kupitia mchezaji wao Jafary Kibaya ambapo mpaka wakati wa kwenda mapumziko matokeo yalikuwa 0-1 licha ya Simba tupambana kusawazisha .

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Simba wakiwa na uchu zaidi wa kufika langoni mwa mpinzani wao licha ya kukutana na upinzani mkali kutoka kwa wachezaji wa timu ya mashujaa ambapo hata hivyo dakika ya 65 ya mchezo huo Leonel Ateba alifungua akaunti ya mabao kwa Simba kupitia mkwaju wa penati na kufanya ubao kusomeka 1-1 na alirejea tena nyavuni kupitia mkwaju wa penati ya pili hivyo kufanya ubao kusomeka 2-1 matokeo yaliyobaki hadi mwisho wa mchezo huo na kuwafanya Simba kubeba alama zote tatu .

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *