SIMBA ‘KUKIWASHA’ NA MASHUJAA LEO LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC inarejea rasmi leo ambapo mchezo mmoja utachezwa katika uwanja wa KMC Complex uliopo Mwenge mkoani Dar es Salaam timu ya Simba ikiikaribisha timu ya Mashujaa kutoka mkoani Kigoma.

Mchezo huo utachezwa majira ya saa kumi jioni ikiwa ni mchezo wa kiporo cha mzunguko wa 24 wa Ligi Kuu ya NBC ambao haukuchezwa kutokana na Simba kuwa na michezo ya Kombe la Shirikisho Afrika ambapo wamefanikiwa kufuzu fainali ya michuano hiyo.

Simba ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 57 ikifanikiwa kufunga mabao 52 na kuruhusu mabao 8 ikiwa ni timu iliyoruhusu mabao machache kuliko timu zote ikiwa timu hiyo imeshacheza michezo 22.

Mashujaa ipo nafasi ya 10 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imefanikiwa  kufunga mabao 26 ikiruhusu mabao 30 katika michezo 26 ambayo timu hiyo imeshacheza.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *