Category: STORY

MBEYA CITY YAREJEA LIGI KUU YA NBC

TIMU ya Mbeya City imerejea rasmi Ligi Kuu ya NBC ambayo ni Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika  wakitokea Ligi ya Championship ya NBC baada ya kufanikiwa kufikisha alama 65 baada ya kuifunga timu ya Cosmopolitan mabao 5-0 huku ikiwa na mchezo mmoja ikiwa ni wiki moja baada ya Mtibwa Sugar kufanikiwa kurejea Ligi Kuu ya NBC.

Mbeya City ilishuka  na sasa wamerejea rasmi huku ikiwa imeweka rekodi ya kufunga mabao mengi ksatika Ligi ya Championship baada ya kufunga mabao 63 katika michezo 29 ambayo timu hiyo imeshacheza mpaka sasa huku katika michezo yao  14 ya nyumbani wakishinda 11 na sare 3 na ugenini  michezo 15 wakishinda michezo nane sare tano na kufungwa michezo miwili

 

Aidha timu hiyo imefanikiwa kufunga mabao 63 kuruhusu mabao 26 katika michezo timu hiyo  iliyocheza huku wakiwa wamebaki na mchezo mmoja ili kuweza kutamatika kwa Ligi ya Championship ya NBC ambao pia utaamua nani bingwa wa Ligi hiyo kati ya Mtibwa Sugar wenye alama 68 au Mbeya City wenye alama 65.

RAIS KARIA

RAIS KARIA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA VIENNA, AISHUKURU FIFA.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia ametoa shukrani kwa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kwa kuichagua Tanzania kuwa miongoni mwa washiriki wa Warsha ya kuimarisha maendeleo ya mpira wa miguu duniani inayohusisha Nchi Wanachama wa UEFA na CAF inayoendelea Vienna, Austria.

Rais Karia amesema ni heshima kwake na shirikisho kushiriki pamoja na mashirikisho mengine kutoka Afrika na Ulaya.

“Ni furaha kuwa miongoni mwa washiriki kwasababu mijadala mingi inasaidia sana na inatupa data za kuweza kuendeleza mpira wa miguu Nchini kwetu”

Amesema kuna haja ya warsha za aina hiyo kuendelea kutolewa zaidi ili kupata maarifa yanayoweza kusaidia katika shughuli za kila siku katika maendeleo ya mpira wa miguu.

Nchi zinazohudhuria kwenye Warsha hiyo ni Finland, Moldova, Wales, Austria, Georgia kutoka UEFA na Gabon, Morocco, Senegal, Tanzania na Cameroon kutoka CAF.

FIRST LEAGUE

HATMA YA KUBAKI FIRST LEAGUE KUAMULIWA LEO.

JIBU la timu gani itaendelea kusalia ligi ya First League msimu wa 2025/2026 litapatikana leo Aprili 30 kwenye michezo ya mzunguko wa pili wa mtoano wa kushuka daraja (Relegation Play Off).

Mapinduzi itaialika Tunduru Korosho kwenye uwanja wa Nyamagana, Mwanza huku Magnet ikiwa mwenyeji wa Copco kwenye uwanja wa Manungu mkoani Morogoro.

Kwenye michezo ya duru la kwanza Tunduru Korosho ilikuwa mwenyeji wa Mapinduzi kwenye uwanja wa Majimaji mkoani Songea mchezo uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2 na Copco iliialika Magnet kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza mchezo uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2.

Timu zitakazopoteza katika matokeo ya jumla (aggregate) zitapata nafasi ya kuendelea kujitetea kwa kucheza na timu mbili zitakazoshika nafasi ya tatu na ya nne kwenye Fainali za mabingwa wa mikoa.

Ratiba ya Ligi Kuu ya NBC 2025/2026

TAARIFA YA KAMATI YA UENDESHAJI NA USIMAMIZI WA LIGI YA BODI YA LIGI KUU TANZANIA (TPLB).

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Aprili 26, 2025 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;

Timu ya Tanzania Prisons ya mkoani Mbeya imepewa adhabu ya Onyo Kali kwa kosa la wawakilishi wa timu kuchelewa kwa dakika 12 kuwasili kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo (MCM) kinyume na matakwa ya kanuni ya 17:2 (2.1).Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 194: Tanzania Prisons 1-0 Kagera Sugar

Klabu ya Tanzania Prisons ya mkoani Mbeya imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la watoto waokota mipira (Ball Kids) kuficha na kuchelewesha kwa makusudi kurejesha mipira kiwanjani.

Kuanzia dakika ya 63 ya mchezo, watoto hao walikuwa wakificha mipira inayotoka hali iliyosababisha hadi kufika dakika ya 80 ya mchezo uwe umesalia mpira mmoja pekee kiwanjani.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 195: Pamba Jiji 1-0 Tabora United

Klabu ya Tabora United ya mkoani Tabora imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kukataa kutumia chumba maalum cha kuvalia kwa kile walichoeleza kuwa kulikuwa na harufu isiyo ya kawaida.

Kamishna pamoja na Mratibu wa mchezo huo waliwasiliana na Daktari wa mchezo ili kuthibitisha hali hiyo lakini aliwaeleza kuwa harufu hiyo ilikuwa ya Sabuni zilizotumika kufanyia usafi katika vyumba vyote (kikiwemo chumba cha timu mwenyeji).Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi Namba 200: Singida BS 1-0 Azam FC

Kocha Mkuu wa Klabu ya Azam FC Rachid Taoussi ameadhibiwa kwa kutozwa faini yaSh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuwafanyia vurugu na kuwarushia chupa ya maji waamuzi wa mchezo tajwa hapo juu mara baada ya mchezo huo kutamatika.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 45:2(2.1) ya ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Makocha.

Mechi Namba 202: Pamba Jiji 1-1 Fountain Gate

Klabu ya Fountain Gate imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la kukataa kutumia chumba maalum cha kuvalia kwa kile walichoeleza kuwa chumba hicho kilikuwa na joto, uamuzi ambao waliufanya bila kumshirikisha Afisa yeyote wa mchezo.Adhabu hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Ligi ya Championship ya NBC

Mechi Namba 195: Green Warriors 2-3 Polisi Tanzania

Klabu ya Polisi Tanzania ya mkoani Kilimanjaro imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la kuchelewa kufika kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo. Meneja wa timu ya Polisi Tanzania Maliki Warioba alifika kwenye kikao saa 4:25 huku viongozi wengine wakifika saa 4:35 badala ya saa 4:00 ambapo walikuta kikao kimefungwa.

Kuchelewa kwenye Kikao cha Maandalizi ya mchezo ni kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo.

Mechi Namba 201: Kiluvya FC 0-1 Mbeya Kwanza

Klabu ya Mbeya Kwanza ya mkoani Mtwara imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la kuwakilishwa na maofisa wanne (4) badala ya watano (5) kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo

Mechi Namba 203: Mtibwa Sugar 2-1 Mbuni FC

Klabu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la maofisa wake wawili kutokuvaa sare za timu kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2(2.10) ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo

Mechi Namba 207: Songea United 1-2 Stand United

Klabu ya Songea United ya mkoani Ruvuma imeadhibiwa kwa kupewa Onyo kali kwa kosa la kuchelewa kuwasili uwanjani. Songea United waliwasili uwanjani saa 8:45 mchana badala ya saa 8:30 mchana kinyume na kanuni ya 17:15 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo

Mechi Namba 214: Geita Gold 2-1 Songea United

Klabu ya Songea United ya mkoani Ruvuma imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la kuchelewa kufika kwenye kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo. Wawakilishi timu ya Songea United walifika kwenye kikao saa 4:07 badala ya saa 4:00.Kuchelewa kwenye Kikao cha Maandalizi ya mchezo ni kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2 ya Championship kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 17:62 ya Championship kuhusu Taratibu za mchezo.

First League

Mechi Namba 54A: Pan African 1-1 Nyumbu FC

Daktari wa klabu ya Nyumbu, Alex Theodory amefungiwa kwa kipindi cha mwezi moja (1) na kutozwa faini ya Sh. 300,000 (laki tatu) kwa kosa la kumtolea lugha ya matusi mwamuzi wa kati wa mchezo tajwa hapo juu.

Daktari huyo alifanya kitendo hicho kisicho cha kiuanamichezo wakati wa mchezo huo na aliadhibiwa pia kwa kadi nyekundu na mwamuzi wa mchezo.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 47:3 ya First League kuhusu Udhibiti kwa Viongozi.

Mechi Namba 56A: Dar City 3-0 Tunduru Korosho

Klabu ya Tunduru Korosho ya mkoani Ruvuma imeadhibiwa kwa kupewa Onyo Kali kwa kosa la wawakilishi wake kushindwa kuhudhuria kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo. Kutokufika kwenye Kikao cha Maandalizi ya mchezo ni kwenda kinyume na Kanuni ya 18:2 (2.2) ya First League kuhusu Taratibu za Mchezo.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 18:60 ya First League kuhusu Taratibu za mchezo.

Mechi Namba PO1: Tunduru Korosho 2-2 Mapinduzi FC

Meneja wa klabu ya Mapinduzi, David Kinasa amefungiwa kwa kipindi cha mwezi moja (1) na kutozwa faini ya Sh. 300,000 (laki tatu) kwa kosa la kumtolea lugha ya matusi mwamuzi wa mchezo.

Kinasa alifanya kitendo hicho kisicho cha kiuanamichezo wakati wa mchezo huo na aliadhibiwa pia kwa kadi nyekundu.Adhabu hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 47:3 ya First League kuhusu Udhibiti kwa Viongozi.

 

 

MTIBWA SUGAR ‘WABABE’ WA NYUMBANI NBC CHAMPIONSHIP

LIGI ya Championship ya NBC imeendelea kwa mzunguko wa 28 ambapo Mtibwa Sugar inaongoza kwa kushinda mechi iliyocheza nyumbani katika uwanja wa Manungu Complex ikishinda mechi zote 14, huku ikifanikiwa kupanda daraja kwenda Ligi Kuu ya NBC ikiwa  na alama 67 hadi sasa.

Geita Gold imeshinda michezo 13 iliyocheza uwanja wa nyumbani wa Nyankumbu huku timu hiyo ikishika nafasi ya nne baada ya kukusanya alama 54.

Nafasi ya tatu inashikwa na Stand United iliyoshinda michezo 12 katika uwanja wa Kambarage  uliopo mkoani Shinyanga ikishika nafasi ya tatu pamoja na kukusanya alama 59.

Mbeya City imefanikiwa kushinda michezo 10 katika uwanja wa  Sokoine mkoani Mbeya  huku ikiwa katika nafasi ya pili  kwenye msimamo wa Ligi ya NBC Championship ikikusanya alama 62 sawa na TMA iliyoshinda michezo 10 katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.

Kwa upande wa  timu ya Bigman  iliyopo nafasi ya saba kwenye msimamo ikiwa na alama 46 ikiwa imeshinda michezo tisa katika uwanja wa Ilulu uliopo mkoani Lindi.

Mbeya Kwanza na Songea United zimefanikiwa kushinda michezo nane kila timu katika  viwanja vyao vya nyumbani ambavyo ni Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara kwa upande wa Mbeya Kwanza na Majimaji mkoani Songea kwa upande wa Songea United.